MABADILIKO YA TAREHE YA KUFUNGUA SHULE

02 Sep 2022

MABADILIKO YA TAREHE YA KUFUNGUA SHULE

Ndugu mzazi salamu,

YAH: MABADILIKO YA TAREHE YA KUFUNGUA SHULE

Leo tarehe 02/09/2022 Shule imepokea taarifa ya mabadiliko ya tarehe ya kufungua shule kutoka kwa OR-TAMISEMI  Kuwa Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa mashindano ya wanafunzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kati (FEASSA). Mashindano hayo yatafanyika katika mkoa wa Arusha. Miongoni mwa taasisi zilizochaguliwa kuwapa malazi wanamichezo ni shule yetu ya TRUST ST PATRICK. Hivyo basi, shule zitafunguliwa kama ifuatavyo:-

1.    Wanafunzi wote wa bweni kuanzia chekechea  mpaka darasa  la sita wataripoti shuleni  tarehe 25/09/2022.

2.    Wanafunzi wote wa kutwa(day) kuanzia chekechea mpaka darasa la sita wataripoti tarehe 26/09/2022.

3.    Likizo ya nusu muhula iliyotakiwa kuanza tarehe  30/09/2022 hadi tarehe 10/10/2022 HAITAKUWEPO ili kufidia siku ambazo zimetumika kwa michezo.

Shule itakapofunguliwa tarehe 26/09/2022 haitafungwa mpaka tarehe 08/12/2022