MASHINDANO YA MICHEZO YA SHULE ZA AFRIKA MASHARIKI (FEASSSA) YATAKAYOFANYIKA MWEZI SEPTEMBA, 2022.

02 Sep 2022

MASHINDANO YA MICHEZO YA SHULE ZA AFRIKA MASHARIKI (FEASSSA) YATAKAYOFANYIKA MWEZI SEPTEMBA, 2022.

YAH: MASHINDANO YA MICHEZO YA SHULE ZA AFRIKA

MASHARIKI (FEASSSA) YATAKAYOFANYIKA MWEZI SEPTEMBA, 2022.

 

Tafadhali husika na mada tajwa hapo juu

2. Mashindano ya Michezo yanayohusisha wanamichezo kutoka nchi

wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEASSSA) yatafanyika Mkoani

Arusha kuanzia tarehe 10-24 Septemba, 2022.

3. Mashindano haya yatahusisha Wanamichezo zaidi ya elfu nne (4000) kutoka

katika nchi hizo.

4. li kufanikisha mashindano haya muhimu, unaombwa kushiriki kikamilifu katika

maandalizi ya mapokezi ya wageni wa mashindano haya ikiwa ni pamoja na Shule

yako kutumika kama Kituo cha kulaza wanamichezo tarajiwa.

5. Kutokana na Shule yako kuwa kituo cha kulaza Wanamichezo hao,

utalazimika kufunga Shule kwa muda huo hadi Michezo itakapomalizika,

isipokuwa kwa Madarasa ya Mitihani ya Taifa. Aidha Shule husika

zitafunguliwa tarehe 26/09/2022. Siku zilizotumika wakati wa FEASSSA zifidiwe

wakati wa likizo ya mwezi Disemba, 2022.

6. Waraka wa Elimu Na.1 na 2 wa Mwaka 2022 kuhusu Kalenda ya Mihula ya

masomo kwa Shule za Awali, Msingi, Sekondari pamoja na kidato cha Tano na Sita

umeambatishwa kwa rejea.